Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu ametaka kuvunjwa kwa Muungano. Nimetuma maoni yafuatayo kwenye gazeti la Mwananchi. 
Maoni ya mwakilishi wa CUF Jussa yanabidi ya kemewe sio tu na chama chake 
bali na watu wote wa Tanzania Bara na Visiwani. Maoni ya uchochezi 
yasiyo na msingi hayapaswi kuvumiliwa. Kiongozi yeyote ambaye anasimama 
mbele ya watu na kusema muungano haupaswi kuwepo ilhali takwimu za 
utafiti wa Tume ya Katiba inaonyesha idadi kubwa ya watu wa Tanzania 
wanataka muungano uwepo anapaswa kutoltiliwa maanani. Chama cha CUF 
kinapaswa kutoa tamko na kuhusiana na kauli ya Bw. Jussa! Watanzania 
wameainisha mstakabali wao kupitia rasimu ya awali ya Katiba. Sasa 
mjadala sio uwepo wa muungano bali mfumo na uthabiti wa muundo wa 
muungano. Tusikubali watu walio na maslahi binafsi ya uongozi 
kuturudisha nyuma.
 
 
No comments:
Post a Comment