Monday 6 January 2014

Maoni kuhusiana na Mgogoro ndani ya Chadema

Kufuatia mgogoro mzito ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), nimetuma maoni yafutayo kwenye gazeti la Mwananchi. Chini ya kichwa cha habari Chadema yamtimua Dk. Kitila, Mwigamba.

Demokrasia ndani ya vyama vya siasa ni suala ngeni na gumu hususan katika nchi yetu ya Tanzania. Kwa nchi kama yetu ambayo tumekulia na kulelewa katika mfumo wa chama kimoja na kutawaliwa na chama kimoja kwa muda mzima wa uhuru wetu, utamaduni wa siasa ya vyama vingi bado hujakita mzizi licha ya mabadiliko katika katiba mwanzoni mwa miaka ya 90. Minghairi ya hayo, yanayotokea Chadema ni moja wapo ya michakato ya upevu na upanuzi wa mjadala wa demokrasia nchini. Kunao wanakubalina na kunao wanapinga yanayotokea Chadema. Tuyachukulie yanayojiri ndani ya Chadema kama hatua moja wapo katika demokrasia. Demokrasia, msingi wake ukiwa katika vyama na asasi mbali mbali inajengwa kwa muda mrefu na sio rahisi. Hatua tuliyofika ya vyombo vya habari na umma kujadili kwa hisia kubwa yanayojiri ndani ya Chadema ni hatua nzuri. Tusiyachukulie tu hivi hivi bali tuombe pia vyama vingine vipate kujadili wanachama wao, kujadili mada za kitaifa na mustakabali wa nchi yetu kwa ari kama hii. Upanuzi wa mijadala ndio msingi wa demokrasia. Mungu ibariki Tanzania.

[ZELEZA] Malawi’s Political Earthquake: Nullification of the Presidential Elections

By Prof Paul Tiyambe Zeleza  3/2/2020 The Malawian Constitutional Court has annulled last year's presidential election results....

Most Viewed