Friday 16 November 2012

Iranians to hold nationwide anti-Israeli demo

Via Press TV
Iran's Islamic Publicity Coordination Council has called on the Iranian people to take part in nationwide demonstrations to condemn Israeli aggression against the Palestinians in the besieged Gaza Strip. The demonstrations are set to be held across the country after Friday Prayers.
 
In a statement issued on Thursday, the council condemned the latest wave of Israeli attacks on the coastal enclave, calling on the Iranians to take to the streets to vent their anger at the fake Zionist regime of Israel and to express their sympathy with the oppressed people of the Gaza Strip.  At least 21 people have been killed and over 160 others injured in the new wave of attacks on the costal sliver, which started on Wednesday.
 

Wednesday 14 November 2012

Sababu Tano za Gor Mahia kuukosa ubingwa

Nicodemus Minde, Nairobi
Kiu ya ukata wa ligi kuu Kenya kwa timu ya Gor Mahia inaendelea. Ni miaka 18 tangu wautwae ubingwa wa Kenya. Kiu hii ilikua ikatwe kwa Gor kuifunga Thika United kwani walikua wanaongoza ligi kwa pointi moja. Licha ya hilo, Gor walikua walikuwa wanakamilisha ratiba ya mechi kwenye uwanja wao wakihistoria wa City Stadium na kwa maoni ya mashabiki wengi walikua wanakutana na timu ambayo isingewaumiza kichwa hata kidogo. Timu ya Thika United sio timu ambayo Gor Mahia wangeihofia sana. Isitoshe walikuwa washaifunga AFC Leopards na Tusker ambazo nazo zilikua zinawania ubingwa. Kibarua cha kuifunga Thika United kilikuwa kidogo sana ukilinganisha na mtihani wao dhdi ya AFC Leopards na Tusker. Mashabiki wa Gor walitamba kwamba kiu ya ubingwa ingeisha kwa kuifunga Thika United kiulaini kwenye uga wa City. Lakini wapi! Gor walilazimisha sare na timu ‘dhaifu’ ya Thika United na Tusker wakashinda hivyo kutetea ubingwa. Zipate sababu tano za Gor Mahia kukosa ubingwa.
1.       1. Presha ya Mechi
Licha ya kuongoza ligi na kuingia katika mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Thika United na mmoja wa mastraika hatari, Danny Ssserukuma, Gor Mahia walikuwa na presha kubwa sana. Ni miaka kumi na saba tangu Gor watwae ubingwa wa ligi kuu Kenya. Licha ya matokeo mazuri mwishoni mwa ligi, Gor Mahia walijikuta na presha nyingi. Kulikua na presha ya mashabiki, presha ya kuleta ubingwa baada ya miaka mingi ya ukata, presha yakurudisha hadhi ya timu ya Gor Mahia n.k. Ilikuwa ni wazi kwamba mambo haya yalicheza kwenye saikolojia ya wachezaji wa Gor hivyo lukosa ubingwa.
2.      2.Kupanick kwa Logarusic
Kocha wa Gor Mahia alikuwa na presha nyingi kwenye mechi ya mwisho dhidi ya Thika United. Alikua hajatulia hata kidogo. Alikua anamhemko na hakutulia kwenye benchi. Alifanya mambo kwa pupa sana. Dhihirisho tosha ni pale alipofanya mabadiliko mapema alipoona mabo hayaendi sawa kwenye kipindi cha kwanza. Licha ya mabadiliko hayo kuleta uhai na afueni kidogo, kipindi cha pili pia alifanya mabadiko ya pupa mno. Mechi kama hizi, kocha anapaswa kutulia kwenye benchi akitoa mawaidha kidogo kwani wachezaji wanajua fika shughuli pevu inayowakabili.
3.      3. Matano kucheza “Mind-games”
Kocha wa Manchester United Sir Alex Ferguson ndio mtaalamu wa kuwachezea makocha wa timu pinzani mchezo wa akili (mind-games). Mchezo huu unasaidia sana kuvuruga mipango ya kocha wa timu pinzani. Kocha wa Tusker Robert Matano aliulizwa baada ya kufungwa na Gor Mahia mstakabali wa ligi. Alijibu kwa maneno machache na kusema ligi bado haijaisha. Hizo zilikuwa wiki mbili zilizopita. Aliendelea kusisitiza kauli hii lich ya kuwa Gor Mahia kuwa kwenye nafasi nzuri ya kushinda ligi zaidi ya timu yake. Alipohojiwa tena kwenye runinga ya Super Sports, Matano aliendelea kusisitiza kwamba bado ligi ni mbichi na timu yake itapambana hadi mwisho. Msimamo huu uliiweka Gor Mahia kwenye presha kubwa, wakijua wakiteleza tu, ligi inawaponyoka. Gor walipoteleza kwa kulazimishwa sare na Tusker walihifadhi taji lao kwa kuibamiza City Stars.
4.      4. Mashabiki kujiamini mno
Mashabiki wa Gor Mahia wanatambulika kwa tambo zao. Wanambwebwe nyingi sana. Wanaipenda timu yao sana. Ni jambo zuri sana kwa timu kuwa na mashabiki wa namna hii. Wachezaji wanapata motisha kubwa kutokana na ushabiki huu. Kabla ya mechi yao na Thika United, mashabiki wa Gor walionekana jijini Nairobi wakiwa wameandika jezi zao “Mabingwa 2012”. Wengi wao waliweka nembo ya kombe la ligi kwenye mashati yao huku wengine wakibeba kombe bandia la ligi. Sio vibaya kujiamini. Inaeleweka kwenye soka, lakini kujiamini huku kuliwatia wachezaji presha kubwa sana. Ndio hivo, baada ya mechi wengi walijawa na majonzi na simanzi kubwa baada ya Gor kuukosa ubingwa.
5.      5. Soka safi la Thika United
Wengi wanachambua udhaifu wa Gor kwenye mechi yao ya mwisho na wanaisahau Thika United. Thika United walicheza bila presha yoyote. Walitandaza soka safi na la kuburudisha. Walipiga pasi nyingi na kuwanyima Gor mpira kwa muda mrefu. Hawakupaki basi kama timu nyingi hufanya zinavyocheza na Barcelona. Walionana vema sana. Walipotangulia kufunga goli ndipo mpira wa ukahimarika zaidi. Walipiga pasi fupi fupi huku mastraika wao wakiisumbua ngome ya Gor Mahia mara kwa mara. Walipiga mashambulizi mengi ya kushtukizia pia. Kwa mpira huu, Gor walishindwa kuivunja ngome ya Thika.

[ZELEZA] Malawi’s Political Earthquake: Nullification of the Presidential Elections

By Prof Paul Tiyambe Zeleza  3/2/2020 The Malawian Constitutional Court has annulled last year's presidential election results....

Most Viewed