Friday 31 January 2014

Kauli ya Jussa Ladhu ya kuvunja Muungano haistahili na inapaswa kukemewa!

Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF), Ismail Jussa Ladhu ametaka kuvunjwa kwa Muungano. Nimetuma maoni yafuatayo kwenye gazeti la Mwananchi.

Maoni ya mwakilishi wa CUF Jussa yanabidi ya kemewe sio tu na chama chake bali na watu wote wa Tanzania Bara na Visiwani. Maoni ya uchochezi yasiyo na msingi hayapaswi kuvumiliwa. Kiongozi yeyote ambaye anasimama mbele ya watu na kusema muungano haupaswi kuwepo ilhali takwimu za utafiti wa Tume ya Katiba inaonyesha idadi kubwa ya watu wa Tanzania wanataka muungano uwepo anapaswa kutoltiliwa maanani. Chama cha CUF kinapaswa kutoa tamko na kuhusiana na kauli ya Bw. Jussa! Watanzania wameainisha mstakabali wao kupitia rasimu ya awali ya Katiba. Sasa mjadala sio uwepo wa muungano bali mfumo na uthabiti wa muundo wa muungano. Tusikubali watu walio na maslahi binafsi ya uongozi kuturudisha nyuma.

No comments:

Post a Comment

[ZELEZA] Malawi’s Political Earthquake: Nullification of the Presidential Elections

By Prof Paul Tiyambe Zeleza  3/2/2020 The Malawian Constitutional Court has annulled last year's presidential election results....

Most Viewed